1 Haya, shuka, keti mavumbini,Ewe bikira, binti Babeli;Keti chini pasipo kiti cha enzi,Ewe binti wa Wakaldayo;Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.
2 Twaa mawe ya kusagia, usage unga;Vua utaji wako, ondoa mavazi yako,Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.
3 Uchi wako utafunuliwa,Naam, aibu yako itaonekana.Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.
4 Mkombozi wetu, BWANA wa majeshi ndilo jina lake,Mtakatifu wa Israeli.
5 Kaa kimya, ingia gizani,Ee binti wa Wakaldayo;Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.