Amosi 9 BHN

Adhabu ya Mungu

1 Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama kando ya madhabahu, naye akaniamuru:“Zipige hizo nguzo za hekalumpaka misingi yake itikisike.Zivunje hizo nguzo ziwaangukie watu vichwani.Wale watakaosalia nitawaua kwa upanga;hakuna hata mmoja wao atakayenusurika,naam, hakuna atakayetoroka.

2 Wajapojichimbia njia ya kwenda kuzimu,huko nitawachukua kwa mkono wangu;wajapopanda mbinguni,nitawaporomosha chini.

3 Wajapojificha juu ya mlima Karmeli,huko nitawasaka na kuwachukua;wajapojificha mbali nami vilindini mwa bahari,humo nitaliamuru joka la baharini liwaume.

4 Wajapochukuliwa mateka na adui zao,huko nitatoa amri wauawe kwa upanga.Nitawachunga kwa makini sananiwatendee mabaya na si mema.”

5 Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi,anaigusa ardhi nayo inatetemekana wakazi wake wanaomboleza;dunia nzima inapanda na kushukakama kujaa na kupwa kwa mto Nili wa Misri.

6 Mwenyezi-Mungu amejenga makao yake mbinguni,nayo dunia akaifunika kwa anga;huyaita maji ya bahari,na kuyamwaga juu ya nchi kavu.Mwenyezi-Mungu, ndilo jina lake!

Marekebisho baada ya uharibifu

7 Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Kwangu mimi, nyinyi Waisraeli,hamna tofauti yoyote na watu wa Kushi!Niliwatoa Wafilisti kutoka Krete,na Waashuru kutoka Kiri,kama nilivyowatoa nyinyi kutoka Misri.

8 Mimi, Bwana Mwenyezi-Mungu nautazama ufalme wenye dhambi,na nitauangamiza kabisa kutoka duniani.Lakini sitawaangamiza wazawa wote wa Yakobo.

9 “Tazama, nitatoa amri,na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifakama mtu achekechavyo nafakaniwakamate wote wasiofaa.

10 Wenye dhambi miongoni mwa watu wangu,watafia vitani kwa upanga;hao ndio wasemao:‘Maafa hayatatukumba wala kutupata!’

11 “Siku yaja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka;nitazitengeneza kuta zake,na kusimika upya magofu yake.Nitaijenga upya kama ilivyokuwa hapo zamani.

12 Nao Waisraeli watamiliki mabaki ya Edomuna mataifa yote yaliyokuwa yangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema,na nitafanya hivyo.

13 “Wakati waja kwa hakika,ambapo mara baada ya kulimamavuno yatakuwa tayari kuvunwa;mara baada ya kupanda mizabibuutafuata wakati wa kuvuna zabibu.Milima itabubujika divai mpya,navyo vilima vitatiririka divai.

14 Nitarekebisha hali ya watu wangu Waisraeli.Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi humo;watapanda mizabibu na kunywa divai yake;watalima mashamba na kula mazao yake.

15 Nitawasimika katika nchi yao,wala hawatang'olewa tenakutoka katika nchi niliyowapa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Sura

1 2 3 4 5 6 7 8 9