1 Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na mbili, mwaka wa kumi na mbili tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2 “Wewe mtu! Imba utenzi wa kuomboleza juu ya Farao, mfalme wa Misri.Wewe Farao unajiona kuwa simba kati ya mataifa,lakini wewe ni kama mamba tu majini:Unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako,wayavuruga maji kwa miguu yako,na kuichafua mito.
3 Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema:Nitautupa wavu wangu juu yako,nao watu watakuvua humo kwa wavu wangu.
4 Nitakutupa juu ya nchi kavu,nitakubwaga uwanjani,nitawafanya ndege wote watue juu yako,na kuwashibisha wanyama wote wa porini kwa mwili wako.