15 Katika vizazi vyote vijavyo, kanuni zilezile mtakazofuata nyinyi ndizo atakazofuata mgeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi; mbele ya Mwenyezi-Mungu mtakuwa sawa;
16 nyinyi na yeye mtakuwa chini ya sheria ileile moja na maagizo yaleyale.”
17 Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Waeleze
18 Waisraeli kwamba wakati watakapoingia katika nchi ninayowapeleka
19 kila mtakapokula mazao ya nchi hiyo, mtatenga kiasi fulani na kunipa mimi Mwenyezi-Mungu.
20 Mtakapooka mikate, mkate wa kwanza wa mazao ya kwanza ya nafaka yenu utatolewa kama sadaka kutoka mahali pa kupuria nafaka.
21 Mtanitolea mimi Mwenyezi-Mungu sadaka hii maalumu katika vizazi vyenu vyote vijavyo.