53 Mtaichukua nchi hiyo na kukaa humo kwa sababu nimewapeni muimiliki.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kura kufuata familia zenu; eneo kubwa kwa kabila kubwa na eneo dogo kwa kabila dogo.
55 Lakini kama msipowafukuza wenyeji wa nchi hiyo kwanza, basi wale mtakaowaacha watakuwa kama vibanzi machoni mwenu au miiba kila upande, na watawasumbua.
56 Nami nitawafanyeni nyinyi kama nilivyokusudia kuwafanya wao.”