6 Basi, nitaiziba njia yake kwa miiba,nitamzungushia ukuta,asipate njia ya kutokea nje.
7 Atawafuata wapenzi wake,lakini hatawapata;naam, atawatafuta,lakini hatawaona.Hapo ndipo atakaposema,“Nitarudi kwa mume wangu wa kwanza;maana hapo kwanza nilikuwa nafuu kuliko sasa.”
8 Hakujua kwamba ni miminiliyempa nafaka, divai na mafuta,niliyemjalia fedha na dhahabu kwa wingi,ambazo alimpelekea Baali.
9 Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaichukua nafaka yangu,nitaiondoa divai yangu wakati wake.Nitamnyang'anya nguo zangu za sufu na kitani,ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.
10 Nitamvua abaki uchi mbele ya wapenzi wake,wala hakuna mtu atakayeweza kunizuia.
11 Nitazikomesha starehe zake zote,sikukuu zake za mwezi mwandamo na za Sabato,na sikukuu zote zilizoamriwa.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini,anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake.Nitaifanya iwe misitu,nao wanyama wa porini wataila.