1 “Haya! Sikilizeni enyi makuhani!Tegeni sikio, enyi Waisraeli!Sikilizeni enyi ukoo wa kifalme!Nyinyi mlipaswa kuzingatia haki,badala yake mmekuwa mtego huko Mizpa,mmekuwa wavu wa kuwanasa huko Tabori.
2 Mmechimba shimo refu la kuwanasa huko Shitimu.Lakini mimi nitawaadhibuni nyote.
3 Nawajua watu wa Efraimu,Waisraeli hawakufichika kwangu.Nyinyi watu wa Efraimu mmefanya uzinzi,watu wote wa Israeli wamejitia najisi.
4 “Matendo yao yanawazuia wasimrudie Mungu wao.Mioyoni mwao wamejaa uzinzi;hawanijui mimi Mwenyezi-Mungu.
5 Kiburi cha Waisraeli chaonekana wazi;watu wa Efraimu watajikwaa katika hatia yao,nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.
6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe,kumtafuta Mwenyezi-Mungu;lakini hawataweza kumpata,kwa sababu amejitenga nao.
7 Wamevunja uaminifu kwa Mwenyezi-Mungu,wamezaa watoto walio haramu.Mwezi mwandamo utawaangamiza,pamoja na mashamba yao.