10 Kisha utafanya vitanzi hamsini upindoni mwa pazia la mwisho la kipande cha kwanza, na vitanzi hamsini upindoni mwa pazia la mwisho la kipande cha pili.
11 Utatengeneza kulabu hamsini za shaba na kuziingiza katika vile vitanzi hamsini ili kuunganishia vile vipande viwili vya mapazia na hivyo kufanya pazia moja la hema.
12 Ile nusu ya pazia iliyobaki utaitundika upande wa nyuma wa hema.
13 Nusu mita ya urefu wa mapazia iliyo ya ziada utaikunja ininginie pande zote mbavuni mwa hema ili kulifunika.
14 Utatengeneza pia kifuniko kingine cha hema kilichofanywa kwa ngozi laini ya kondoo dume na ngozi laini ya mbuzi.
15 “Utatengeneza mbao za mjohoro za kusimama wima kwa ajili ya hema.
16 Kila ubao utakuwa na urefu wa mita 4, na upana wa sentimita 66.