21 watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.
22 Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli.
23 Hukuniletea wana-kondoo kuwa kafara zako, wala hukuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukutumikisha kwa matoleo, wala sikukuchosha kwa ubani.
24 Hukuninunulia manukato kwa fedha, wala hukunishibisha kwa mafuta ya sadaka zako; bali umenitumikisha kwa dhambi zako, umenichosha kwa maovu yako.
25 Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
26 Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.
27 Baba yako wa kwanza alifanya dhambi, na wakalimani wako wameniasi.