1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;
3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.
4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na hadhari;
5 mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.