4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na hadhari;
5 mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.
6 Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao.
7 Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako,Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako,Na mikufu shingoni mwako.
10 Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi,Wewe usikubali.