28 Matumaini yao wenye haki yatakuwa furaha;Bali kutaraji kwao wasio haki kutapotea.
29 Njia ya BWANA ni kimbilio lake mtu mkamilifu;Bali ni uharibifu kwao watendao maovu.
30 Mwenye haki hataondolewa milele;Bali wasio haki hawatakaa katika nchi.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima;Bali ulimi wa ukaidi utakatiliwa mbali.