6 Baraka humkalia mwenye haki kichwani;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.
7 Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.
8 Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
9 Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.
10 Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
11 Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,
12 Kuchukiana huondokesha fitina;Bali kupendana husitiri makosa yote.