2 Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3 Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4 Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5 Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6 Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7 Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.