20 Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21 Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote;Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22 Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA;Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23 Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa;Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24 Mkono wa mwenye bidii utatawala;Bali mvivu atalipishwa kodi.
25 Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha;Bali neno jema huufurahisha.
26 Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake;Bali njia ya wasio haki huwakosesha.