8 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9 Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12 Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13 Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14 Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.