19 Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.
20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima;Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
21 Uovu huwaandamia wenye dhambi;Bali mwenye haki atalipwa mema.
22 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi;Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.
23 Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini;Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.
24 Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe;Bali yeye ampendaye humrudi mapema.