1 Jawabu la upole hugeuza hasira;Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2 Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3 Macho ya BWANA yako kila mahali;Yakimchunguza mbaya na mwema.
4 Ulimi safi ni mti wa uzima;Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5 Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6 Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7 Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.