11 Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12 Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13 Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15 Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16 Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17 Chakula cha mboga penye mapendano;Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.