20 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21 Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22 Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23 Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.
25 BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26 Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.