22 Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23 Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.
25 BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26 Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.
27 Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;Bali achukiaye zawadi ataishi.
28 Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.