8 Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9 Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10 Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11 Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12 Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13 Moyo wa furaha huchangamsha uso;Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.