8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;Kila kigeukapo hufanikiwa.
9 Afunikaye kosa hutafuta kupendwa;Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.
10 Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu,Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.
11 Mtu mwovu hataki neno ila kuasi tu;Kwa hiyo mjumbe mkali atatumwa kwake.
12 Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake,Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Yeye arudishaye mabaya badala ya mema,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.
14 Mwanzo wa ugomvi ni kama kutoboa penye maji;Basi acheni ugomvi kabla haujafurika.