1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe;Hushindana na kila shauri jema.
2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu;Ila moyo wake udhihirike tu.
3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia;Na pamoja na aibu huja lawama.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.
5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri;Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.
6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina,Na kinywa chake huita mapigo.