11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.
14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
15 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi;Humleta mbele ya watu wakuu.
17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.