14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
15 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi;Humleta mbele ya watu wakuu.
17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
18 Kura hukomesha mashindano;Hukata maneno ya wakuu.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.