17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
18 Kura hukomesha mashindano;Hukata maneno ya wakuu.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.
21 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;Na wao waupendao watakula matunda yake.
22 Apataye mke apata kitu chema;Naye ajipatia kibali kwa BWANA.
23 Maskini hutumia maombi;Bali tajiri hujibu kwa ukali.