3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia;Na pamoja na aibu huja lawama.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.
5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri;Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.
6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina,Na kinywa chake huita mapigo.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake,Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo;Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,Ni ndugu yake aliye mharabu.