7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake,Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo;Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,Ni ndugu yake aliye mharabu.
10 Jina la BWANA ni ngome imara;Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.