11 Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
12 Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
13 Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
14 Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
15 Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
16 Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
17 Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.