4 Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi;Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
5 Mashauri ya moyoni ni kama kilindi;Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.
6 Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe;Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?
7 Mwenye haki aendaye katika unyofu wake,Watoto wake wabarikiwa baada yake.
8 Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu,Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
9 Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu;Nimetakasika dhambi yangu?
10 Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali,Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.