25 Matakwa yake mtu mvivu humfisha,Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa;Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.
27 Sadaka ya wasio haki ni chukizo;Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!
28 Shahidi wa uongo atapotea;Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.
29 Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu;Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.
30 Hapana hekima, wala ufahamu,Wala shauri, juu ya BWANA.