4 Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANANi utajiri, na heshima, nayo ni uzima.
5 Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu;Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.
6 Mlee mtoto katika njia impasayo,Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
7 Tajiri humtawala maskini,Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
8 Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.
10 Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.