14 Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.
15 Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;
16 Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.
17 Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;
18 Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.
19 Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.
20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.