24 Baba yake mwenye haki atashangilia;Naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia.
25 Na wafurahi baba yako na mama yako;Na afurahi aliyekuzaa.
26 Mwanangu, nipe moyo wako;Macho yako yapendezwe na njia zangu.
27 Kwa maana kahaba ni shimo refu;Na malaya ni rima jembamba.
28 Naam, huotea kama mnyang’anyi;Huwaongeza wenye hila katika wanadamu.
29 Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole?Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno?Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu?Ni nani aliye na macho mekundu?
30 Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo;Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.