20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
21 Kupendelea watu si kwema;Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.
22 Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri;Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.
23 Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali;Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.
24 Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa;Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.
25 Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina;Bali amtumainiye BWANA atawandishwa.
26 Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga;Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.