6 Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri.
7 Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima;Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.
8 Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida,Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
9 Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria,Hata sala yake ni chukizo.
10 Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya,Ataanguka katika rima lake mwenyewe;Bali wakamilifu watarithi mema.
11 Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe;Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.
12 Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi;Bali waovu waondokapo, watu hujificha.