4 Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu;Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
5 Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake,Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
6 Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya;Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
7 Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini;Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
8 Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
10 Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.