12 Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi,Kama vile baba mwanawe ampendezaye.
13 Heri mtu yule aonaye hekima,Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha,Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani,Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.
16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume,Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.
17 Njia zake ni njia za kupendeza sana,Na mapito yake yote ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana;Ana heri kila mtu ashikamanaye naye.