6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri,Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
7 Maana kinywa changu kitasema kweli,Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
8 Maneno yote ya kinywa changu yana haki;Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
9 Yote humwelea yule afahamuye,Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
10 Pokea mafundisho yangu, wala si fedha,Na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani;Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu;Natafuta maarifa na busara.