2 Watu wakamlilia Mose, naye akamwomba Mwenyezi-Mungu na moto huo ukazimika.
3 Kwa hiyo, mahali hapo pakaitwa Tabera, kwa sababu hapo moto wa Mwenyezi-Mungu uliwaka kati ya watu.
4 Miongoni mwa Waisraeli kulikuwa na kundi fulani lililoandamana nao ambalo lilikuwa na hamu kubwa. Waisraeli kwa mara nyingine walilia, wakisema. “Laiti kama tungeweza kupata nyama ya kula!
5 Tunakumbuka, samaki tuliokula kule Misri bila malipo, matango, matikiti, mboga, vitunguu na vitunguu saumu!
6 Lakini sasa nguvu zimetuishia na hakuna chakula kingine isipokuwa hii mana tu!”
7 Mana ilikuwa kama punje za mtama, rangi yake ilikuwa kama ya bedoza.
8 Watu walizungukazunguka na kuikusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia au waliitwanga kwa vinu, halafu waliitokosa vyunguni na kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama ya maandazi yaliyokaangwa kwa mafuta.