4 Mungu akakutana naye. Balaamu akamwambia, “Nimetayarisha madhabahu saba na kutoa kafara fahali mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.”
5 Mwenyezi-Mungu akampa Balaamu maneno atakayosema na kumwambia arudi kwa Balaki.
6 Balaamu akarudi, akamkuta Balaki amesimama palepale karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, pamoja na maofisa wote wa Moabu.
7 Balaamu akamtolea Balaki kauli yake, akasema,“Balaki amenileta hapa kutoka Aramu,naam, mfalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki.‘Njoo uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu,naam, njoo uwalaumu Waisraeli!’
8 Nitamlaanije mtu ambaye Mungu hakumlaani?Nitawalaumuje watu ambao Mwenyezi-Mungu hakuwalaumu?
9 Kutoka vilele vya majabali nawaona;kutoka juu ya milima nawachungulia.Hilo taifa likaalo peke yake,lisilojiona kuwa sawa na mataifa mengine.
10 Nani awezaye kuwahesabu wingi wa watu wa Yakobo,au kukisia umati wa Waisraeli?Nife kifo cha waadilifu,mwisho wangu na uwe kama wao.”