7 “Kadiri makuhani walivyoongezeka,ndivyo wote walivyozidi kuniasi.Basi, nitaigeuza fahari yao kuwa aibu.
8 Wanajishibisha kwa sadaka za watu wangu wenye dhambi.Wana hamu sana ya kuwaona wametenda dhambi.
9 Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani;nitawaadhibu kwa sababu ya mwenendo wao,nitawalipiza matendo yao wenyewe.
10 Watakula, lakini hawatashiba;watazini, lakini hawatapata watoto,kwa sababu wameniacha mimi Mwenyezi-Mungu,na kufuata miungu mingine.
11 “Divai mpya na ya zamanihuondoa maarifa.
12 Watu wangu huomba shauri kutoka kwa mti;kijiti chao cha ramli ndicho kinachowapa kauli.Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha;wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine,wakaniacha mimi Mungu wao.
13 Wanatambikia kwenye vilele vya milima;naam, wanatoa tambiko vilimani,chini ya mialoni, migude na mikwaju,maana kivuli chao ni kizuri.“Kwa hiyo binti zenu hufanya uzinzi,na bibiarusi wenu hufanya uasherati.