15 Waliingia ndani ya safina pamoja na Noa wiliwawili wa kila aina ya viumbe hai.
16 Kila aina yao waliingia, dume na jike, kama Mungu alivyomwamuru Noa. Kisha, Mwenyezi-Mungu akaufunga mlango wa safina nyuma yake Noa.
17 Gharika ilidumu nchini kwa muda wa siku arubaini. Maji yakaongezeka na kuiinua safina, ikaelea juu ya ardhi.
18 Maji yakaendelea kuongezeka zaidi nchini na safina ikaelea juu yake.
19 Maji hayo yakawa mengi sana juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu katika nchi.
20 Yaliongezeka hata kuifunika milima kiasi cha mita saba na nusu.
21 Viumbe wote hai katika nchi wakafa. Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama wa porini, makundi ya viumbe wote katika nchi kavu na wanadamu wote;