21 Kiongozi wao atakuwa mmoja wao,mtawala wao atatokea miongoni mwao.Nitamleta karibu naye atanikaribia;maana, nani anayethubutu kunikaribia kwa nguvu zake?Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
22 Nanyi mtakuwa watu wangu,nami nitakuwa Mungu wenu.”
23 Tazama, dhoruba kali kutoka kwa Mwenyezi-Mungu!Ghadhabu imezuka,kimbunga cha tufanikitamlipukia mtu mwovu kichwani.
24 Hasira ya Mwenyezi-Mungu haitarudi nyuma,mpaka atakapotekeleza na kukamilishamatakwa ya moyo wake.Siku zijazo mtayaelewa vema mambo hayo.