15 Mbona unalia juu ya jeraha lako?Maumivu yako hayaponyeki.Nimekutendea hayo yote,kwa sababu kosa lako ni kubwa,dhambi zako ni nyingi mno.
16 Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa,na maadui zako wote watachukuliwa uhamishoni;wanaokuteka nyara, watatekwa nyara,wanaokuwinda nitawawinda.
17 “Nitakurudishia afya yako,na madonda yako nitayaponya,japo wamekuita ‘Aliyetupwa’,‘Mji Siyoni usio na wa kuutunza!’”
18 Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nitazirudisha tena fanaka za maskani ya Yakobo,na kuyaonea huruma makao yake;mji utajengwa upya juu ya magofu yake,na ikulu ya mfalme itasimama pale ilipokuwa.
19 Humo zitatoka nyimbo za shukranina sauti za wale wanaosherehekea.Nitawaongeza na wala hawatakuwa wachache;nitawafanya waheshimiwe wala hawatadharauliwa.
20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa zamani,jumuiya yao itaimarika mbele yangu,nami nitawaadhibu wote wanaowakandamiza.
21 Kiongozi wao atakuwa mmoja wao,mtawala wao atatokea miongoni mwao.Nitamleta karibu naye atanikaribia;maana, nani anayethubutu kunikaribia kwa nguvu zake?Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.