6 Huyo ni kama kichaka jangwani,hataona chochote chema kikimjia.Ataishi mahali pakavu nyikani,katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
7 “Abarikiwe mtu anayemtegemea Mwenyezi-Mungu,mtu ambaye Mwenyezi-Mungu ndiye tegemeo lake.
8 Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya maji,upenyezao mizizi yake karibu na chemchemi.Hauogopi wakati wa joto ufikapo,majani yake hubaki mabichi.Hauhangaiki katika mwaka wa ukame,na hautaacha kuzaa matunda.
9 “Moyo wa mtu ni mdanganyifu kuliko vitu vyote;hauwezi kuponywa, hakuna awezaye kuuelewa!
10 Mimi Mwenyezi-Mungu hupima akilina kuchunguza mpaka ndani ya moyo wa mtu.Na hivyo humtendea kila mmoja,kulingana na mwenendo wake,kadiri ya matendo yake.”
11 Mtu apataye mali isiyo halalini kama kware akusanyaye makinda ambayo hakuyaangua:Wakati wa kilele cha ujana wake itamchopoka,na mwishoni atakuwa mtu mpumbavu.
12 Kuna kiti cha enzi kitukufukiti kilichoinuliwa juu;huko ndiko mahali petu patakatifu.