9 “Moyo wa mtu ni mdanganyifu kuliko vitu vyote;hauwezi kuponywa, hakuna awezaye kuuelewa!
10 Mimi Mwenyezi-Mungu hupima akilina kuchunguza mpaka ndani ya moyo wa mtu.Na hivyo humtendea kila mmoja,kulingana na mwenendo wake,kadiri ya matendo yake.”
11 Mtu apataye mali isiyo halalini kama kware akusanyaye makinda ambayo hakuyaangua:Wakati wa kilele cha ujana wake itamchopoka,na mwishoni atakuwa mtu mpumbavu.
12 Kuna kiti cha enzi kitukufukiti kilichoinuliwa juu;huko ndiko mahali petu patakatifu.
13 Ee Mwenyezi-Mungu tumaini la Israeli,wote wanaokukataa wataaibishwa;wanaokuacha wewe watatoweka,kama majina yaliyoandikwa vumbini,kwa maana wamekuacha wewe Mwenyezi-Mungu,uliye chemchemi ya maji ya uhai.
14 Uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nami nitapona;uniokoe, nami nitaokoka;maana, wewe ndiwe sifa yangu.
15 Tazama watu wanavyoniambia:“Jambo alilotishia Mwenyezi-Mungu liko wapi?Acha basi lije!”