3 Maana siku zaja ambapo nitawarudishia fanaka zao watu wangu wa Israeli na Yuda na kuwarudisha katika nchi niliyowapa wazee wao, nao wataimiliki. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
4 Haya ndiyo mambo aliyosema Mwenyezi-Mungu kuhusu watu wa Israeli na Yuda:
5 “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kumesikika kilio cha hofusauti ya kutisha wala si ya amani.
6 Jiulizeni sasa na kufahamu:Je, mwanamume aweza kujifungua mtoto?Mbona basi, namwona kila mwanamumeamejishika kiunoni kama mwanamke mwenye utunguna nyuso zao zimegeuka rangi?
7 Kweli, siku hiyo ni kubwa,hakuna nyingine kama hiyo;ni siku ya huzuni kwa watu wa Yakobo;hata hivyo, wataokolewa humo.
8 “Siku hiyo itakapofika, nasema mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, nitaivunja nira iliyo shingoni mwao na kukata minyororo yao.
9 Nao hawatakuwa tena watumwa wa wageni, bali watanitumikia mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, na mfalme wa ukoo wa Daudi ambaye nitawateulia.