8 Je, ulipata kuweko katika halmashauri ya Mungu?au, wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?
9 Unajua kitu gani tusichokijua sisi?Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
10 Miongoni mwetu wapo wazee wenye hekima,wenye miaka mingi kuliko baba yako.
11 Je, faraja anazokupa Mungu ni ndogo mno?Au je, neno lake la upole kwako si kitu?
12 Mbona moyo unakusukuma kukasirikana kutoa macho makali,
13 hata kumwasi Munguna kusema maneno mabaya kama hayo?
14 Mtu ni nini hata aweze kuwa mwadilifu?au yule aliyezaliwa na mwanamke hata aweze kuwa mwema?